BUYUNGU:ACT NA CHADEMA ZAUNGANA KUTWAA JIMBO.
Ambapo kwa pamoja wataangalia mgombea mwenye ushawishi zaidi katika jimbo hilo iwe kutoka ACT Wazalendo au Chadema na kumuweka kuwa mgombea rasmi wa ubunge wa jimbo hilo.
Ambapo amasema ACT Wazalendo watamuunga mkono mgombea wa Chadema au Chadema watamuunga mkono mgombea wa ACT Wazalendo.
“Tunataka kuweka mgombea mmoja anayekubalika na wananchi wa Buyungu na kufanya kampeni kwa pamoja mpaka ushindi.“amesema Zitto Kabwe.
“Huu ni mwanzo wa harakati za kuwa na United Democratic Front dhidi ya ukandamizaji wa Demokrasia nchini na dhidi ya Hali mbaya ya Maisha ya Watu wetu. Umoja wa zaidi ya vyama vya siasa ukihusisha Vyama vya Wafanyakazi, Vyama vya Wakulima, Vyama vya Wafanyabiashara na Wananchi wengine.“amemaliza Zitto.
Jimbo la Buyungu kwa sasa lipo wazi baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo kupitia tiketi ya CHADEMA, Kasuku Samson Bilago kufariki dunia mnamo Mei 25, 2018 .
0 on: "BUYUNGU:ACT NA CHADEMA ZAUNGANA KUTWAA JIMBO."