Game Reviews

Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

NIGERIA:WAFUNGWA WATOROKA BAADA YA GEREZA KUVAMIWA

- No comments
Image result for nigeria prisonsJeshi la Polisi nchini Nigeria linaendesha msako dhidi ya wafungwa zaidi ya 180 waliotoroka kutoka baada gereza kuvamiwa na watu wasiojulikana.
Idadi hiyo ya wafungwa walitoroka baada ya watu wenye silaha kuvamia gereza lililo katikati ya jiji la Minna kwenye jimbo la Niger, Jumapili usiku.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Jenerali Abdulrahman Dabazzau amesema kuwa wafungwa 30 waliojaribu kutoroka walikamatwa lakini 189 hawajulikani walipo. Aidha, maafisa wa jeshi hilo wamedai kuwa huenda idadi ya waliotoroka ikawa ni zaidi ya iliyotajwa awali.
Image result for nigeria prisons“Kati ya 219 waliokuwa wametoroka, tulifanikiwa kuwakamata tena 30,” alisema Rabiu Shuaib, msemaji wa Jeshi la Magereza, hali inayoonesha kuwa wafungwa 189 hawajulikani walipo.
Uvamizi wa magereza hufanyika nchini Nigeria na hutekelezwa na kundi la kigaidi la Boko Haram pamoja na makundi mengine ya kihalifu.
Mamlaka ya Magereza nchini humo imeeleza kuwa upelelezi unaendelea kufanyika kuhusu tukio hilo ili kubaini waliotekeleza uvamizi huo na kuwakamata.

UFARANSA:MAOUNDOU AHITAJIWA NA JESHI LA POLISI NCHINI MALI.

- No comments
Kufuatia ombi lilitolewa na Rais wa Mali, Ibrahim Boubacar Keïta kwa kijana, Mamoudou Gassama ambaye amepata umaarufu baada ya kumuokoa mtoto aliyekuwa amening’inia kwenye kibaraza cha ghorofa ya nne katika jengo refu jijini Paris, Ufaransa watu mbalimbali wametoa maoni yao na kudai kuwa si jambo rahisi kwa kijana huyo aliyepewa umaarufu wa Spiderman kukubali kurudi nchini kwake.
Ambapo mapema jana Rais wa Mali alimtaka Mamoudou Gassama kurejea nchini Mali na kulitumikia jeshi la polisi nchini humo kwani tayari ameshamwandalia nafasi ya kazi katika jeshi la polisi la Mali. https://i1.wp.com/dar24.com/wp-content/uploads/2018/05/mamoudou-gassama-fast-facts-about-malian-spiderman-who-climbed-building-to-save-child-dangling-from-balcony.jpg?w=800
Taarifa hizo ziliwasilishwa na Balozi wa Mali nchini Ufaransa, Toumani Djimé Diallo mara baada ya kuzungumza na kijana huyo katika ofisi za ubalozi wa nchi hiyo na kumpa pongezi kutoka kwa rais wa Mali.
Aidha baadhi ya maoni mbalimbali ya watanzania wamesema Ombi la Rais wa Mali ni sawa na kumwambia msichana wa mjini achague pizza na mchicha wakimaanisha kuwa sio rahisi kwa kijana huyo kukubali kurudi nchini kwake Mali ilihali tayari ameshatambulika nchini ufaransa na kupewa uraia wa nchi hiyo ambao alikuwa akiutafuta kwa muda mrefu.
Hata hivyo mtandaoni tayari zimeanza kuzagaa baadhi ya picha za utani zikionesha watu mbalimbali wakikwaa maghorofa wakidai wanafanya uokoaji ili kupata zali alilopata Mamoudou Gassama.
Ukizingatia tayari Rais Macron amempatia kazi Mamoudou katika Jeshi la Zima moto la Ufaransa, pia amemtunukia medali ya kipekee ya ushujaa kijana huyo na kuwataka raia wote kuiga mfano wake.